Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi Afrika Mashariki (EACOP)
Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi Afrika Mashariki (EACOP)
Imewekwa: 28 January, 2025

Mradi huu unahusisha ujenzi wa bomba la inchi 24 lenye urefu wa kilomita 1,443 lenye uwezo wa kusafirisha mapipa 216,000 ya mafuta ghafi kwa siku kutoka Hoima, Uganda, hadi Chongoleani (Tanga), Tanzania, ili kuwezesha usafirishaji wa Mafuta ghafi ya Uganda hadi soko la kimataifa.
Kituo cha mauzo ya baharini kitajengwa Chongoleani, Tanga. Bomba litapashwa joto zaidi ya 50°C kwa mtiririko rahisi wa mafuta. Mradi huo unatekelezwa na Kampuni ya EACOP yenye wanahisa wafuatao; Total (62%), TPDC (15%), UNOC (15%) na CNOOC (8%). Serikali ya Tanzania na Uganda zinawakilishwa kwa mtiririko huo kupitia kampuni zao za kitaifa za mafuta